Zab. 131 Swahili Union Version (SUV)

Kumtumainia Mungu kwa Utulivu

1. BWANA, moyo wangu hauna kiburi,Wala macho yangu hayainuki.Wala sijishughulishi na mambo makuu,Wala na mambo yashindayo nguvu zangu.

2. Hakika nimeituliza nafsi yangu,Na kuinyamazisha.Kama mtoto aliyeachishwaKifuani mwa mama yake;Kama mtoto aliyeachishwa,Ndivyo roho yangu ilivyo kwangu.