Zab. 6 Swahili Union Version (SUV)

Sala ya Kuponywa Ugonjwa Hatari

1. BWANA, usinikemee kwa hasira yako,Wala usinirudi kwa ghadhabu yako.

2. BWANA, unifadhili, maana ninanyauka;BWANA, uniponye, mifupa yangu imefadhaika.

3. Na nafsi yangu imefadhaika sana;Na Wewe, BWANA, hata lini?

4. BWANA urudi, uniopoe nafsi yangu,Uniokoe kwa ajili ya fadhili zako.

5. Maana mautini hapana kumbukumbu lako;Katika kuzimu ni nani atakayekushukuru?

6. Nimechoka kwa kuugua kwangu;Kila usiku nakieleza kitanda changu;Nalilowesha godoro langu kwa machozi yangu.

7. Jicho langu limeharibika kwa masumbufu,Na kuchakaa kwa sababu yao wanaoniudhi.

8. Ondokeni kwangu, ninyi nyote mtendao uovu;Kwa kuwa BWANA ameisikia sauti ya kilio changu.

9. BWANA ameisikia dua yangu;BWANA atayatakabali maombi yangu.