1. Mpeni BWANA, enyi wana wa Mungu,Mpeni BWANA utukufu na nguvu;
2. Mpeni BWANA utukufu wa jina lake;Mwabuduni BWANA kwa uzuri wa utakatifu.
3. Sauti ya BWANA i juu ya maji;Mungu wa utukufu alipiga radi;BWANA yu juu ya maji mengi.
4. Sauti ya BWANA ina nguvu;Sauti ya BWANA ina adhama;
5. Sauti ya BWANA yaivunja mierezi;Naam, BWANA aivunja-vunja mierezi ya Lebanoni;
6. Airusha-rusha kama ndama wa ng’ombe;Lebanoni na Sirioni kama mwana-nyati.
7. Sauti ya BWANA yaipasua miali ya moto;
8. Sauti ya BWANA yalitetemesha jangwa;BWANA alitetemesha jangwa la Kadeshi.
9. Sauti ya BWANA yawazalisha ayala,Na kuifichua misitu;Na ndani ya hekalu lakeWanasema wote, Utukufu.
10. BWANA aliketi juu ya Gharika;Naam, BWANA ameketi hali ya mfalme milele.