1. Nalifurahi waliponiambia,Na twende nyumbani kwa BWANA.
2. Miguu yetu imesimamaNdani ya malango yako, Ee Yerusalemu.
3. Ee Yerusalemu uliyejengwaKama mji ulioshikamana,
4. Huko ndiko walikopanda kabila,Kabila za BWANA;Ushuhuda kwa Israeli,Walishukuru jina la BWANA.
5. Maana huko viliwekwa viti vya hukumu,Viti vya enzi vya mbari ya Daudi.
6. Utakieni Yerusalemu amani;Na wafanikiwe wakupendao;
7. Amani na ikae ndani ya kuta zako,Na kufanikiwa ndani ya majumba yako.
8. Kwa ajili ya ndugu zangu na rafiki zanguNiseme sasa, Amani ikae nawe.