1. Wewe, MUNGU, Bwana wetuJinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!Wewe umeuweka utukufu wako mbinguni;
2. Vinywani mwa watoto wachanga na wanyonyaoUmeiweka misingi ya nguvu;Kwa sababu yao wanaoshindana nawe;Uwakomeshe adui na mijilipiza kisasi.
3. Nikiziangalia mbingu zako, kazi ya vidole vyako,Mwezi na nyota ulizoziratibisha;
4. Mtu ni kitu gani hata umkumbuke,Na binadamu hata umwangalie?
5. Umemfanya mdogo punde kuliko Mungu;Umemvika taji ya utukufu na heshima;
6. Umemtawaza juu ya kazi za mikono yako;Umevitia vitu vyote chini ya miguu yake.
7. Kondoo, na ng’ombe wote pia;Naam, na wanyama wa kondeni;
8. Ndege wa angani, na samaki wa baharini;Na kila kipitacho njia za baharini.