Zab. 127 Swahili Union Version (SUV)

Baraka za Mungu Nyumbani

1. BWANA asipoijenga nyumbaWaijengao wafanya kazi bure.BWANA asipoulinda mjiYeye aulindaye akesha bure.

2. Kazi yenu ni bure, mnaoamka mapema,Na kukawia kwenda kulala,Na kula chakula cha taabu;Yeye humpa mpenzi wake usingizi.

3. Tazama, wana ndio urithi wa BWANA,Uzao wa tumbo ni thawabu.

4. Kama mishale mkononi mwa shujaa,Ndivyo walivyo wana wa ujanani.