Zab. 54 Swahili Union Version (SUV)

Sala ya Uthibitisho

1. Ee Mungu, kwa jina lako uniokoe,Na kwa uweza wako unifanyie hukumu.

2. Ee Mungu, uyasikie maombi yangu,Uyasikilize maneno ya kinywa changu.

3. Kwa maana wageni wamenishambulia;Watu watishao wananitafuta nafsi yangu;Hawakumweka Mungu mbele yao.

4. Tazama, Mungu ndiye anayenisaidia;Bwana ndiye anayenitegemeza nafsi yangu.

5. Atawarudishia adui zangu ubaya wao;Uwaangamize kwa uaminifu wako.

6. Kwa ukunjufu wa moyo nitakutolea dhabihu;Ee BWANA, nitalishukuru jina lako, maana ni jema.