1. Ee Mungu, uniokoe,Ee BWANA, unisaidie hima.
2. Waaibike, wafedheheke,Wanaoitafuta nafsi yangu.Warudishwe nyuma, watahayarishwe,Wapendezwao na shari yangu.
3. Warudi nyuma, na iwe aibu yao,Wanaosema, Ewe! Ewe!
4. Washangilie, wakufurahie,Wote wakutafutao.Waupendao wokovu wakoWaseme daima, Atukuzwe Mungu.