Isa. 60:13-21 Swahili Union Version (SUV)

13. Utukufu wa Lebanoni utakujia wewe,Mberoshi na mtidhari na mteashuri pamoja;Ili kupapamba mahali pangu patakatifu,Nami nitapatukuza mahali pa miguu yangu.

14. Na wana wa watu wale waliokutesaWatakuja kwako na kukuinamia;Nao wote waliokudharauWatajiinamisha hata nyayo za miguu yako;Nao watakuita, Mji wa BWANA,Sayuni wa Mtakatifu wa Israeli.

15. Na kwa kuwa umeachwa na kuchukiwa,Hata ikawa hapana mtu aliyepita ndani yako,Nitakufanya kuwa fahari ya milele,Furaha ya vizazi vingi.

16. Utanyonya maziwa ya mataifa,Utanyonya matiti ya wafalme;Nawe utajua ya kuwa mimi, BWANA, ni mwokozi wako,Na mkombozi wako, Mwenye enzi wa Yakobo.

17. Badala ya shaba nitaleta dhahabu,Na badala; ya chuma nitaleta fedha,Na badala ya mti, shaba,Na badala ya mawe, chuma;Tena nitawafanya wasimamizi wako wawe amani,Na hao wakutozao fedha kuwa haki.

18. Jeuri haitasikiwa tena katika nchi yako,Ukiwa na uharibifu hazitakuwa mipakani mwako;Bali utaziita kuta zako, Wokovu,Na malango yako, Sifa.

19. Jua halitakuwa nuru yako tena wakati wa mchana,Wala mwezi hautakupa nuru kwa mwangaza wake;Bali BWANA atakuwa nuru ya milele kwako,Na Mungu wako atakuwa utukufu wako.

20. Jua lako halitashuka tena,Wala mwezi wako hautajitenga;Kwa kuwa BWANA mwenyewe atakuwa nuru yako ya milele;Na siku za kuomboleza kwako zitakoma.

21. Watu wako nao watakuwa wenye haki wote,Nao watairithi nchi milele;Chipukizi nililolipanda mimi mwenyewe,Kazi ya mikono yangu mwenyewe,Ili mimi nitukuzwe.

Isa. 60