Omb. 2:3-14 Swahili Union Version (SUV)

3. Ameikata pembe yote ya IsraeliKatika hasira yake kali;Ameurudisha nyuma mkono wake wa kuumeMbele ya hao adui,Naye amemteketeza Yakobo kama moto uwakao,Ulao pande zote.

4. Ameupinda upinde wake kama adui,Amesimama na mkono wake wa kuume kama mtesi;Naye amewaua hao woteWaliopendeza macho;Katika hema ya binti SayuniAmemimina kani yake kama moto.

5. Bwana amekuwa mfano wa adui,Amemmeza Israeli;Ameyameza majumba yake yote,Ameziharibu ngome zake;Tena amemzidishia binti YudaMatanga na maombolezo.

6. Naye ameondoa maskani yake kwa nguvu,Kana kwamba ni ya bustani tu;Ameziharibu sikukuu zake;BWANA amezisahauzisha katika SayuniSikukuu za makini na sabato;Naye amewadharau mfalme na kuhaniKatika uchungu wa hasira yake.

7. Bwana ameitupilia mbali madhabahu yake,Amepachukia patakatifu pake;Amezitia katika mikono ya hao aduiKuta za majumba yake;Wamepiga kelele ndani ya nyumba ya BWANAKama katika siku ya kusanyiko la makini.

8. BWANA amekusudia kuuharibuUkuta wa binti Sayuni;Ameinyosha hiyo kamba,Hakuuzuia mkono wake usiangamize;Bali amefanya boma na ukuta kuomboleza;Zote pamoja hudhoofika.

9. Malango yake yamezama katika nchi;Ameyaharibu makomeo yake na kuyavunja;Mfalme wake na wakuu wake wanakaaKati ya mataifa wasio na sheria;Naam, manabii wake hawapati maonoYatokayo kwa BWANA.

10. Wazee wa binti Sayuni huketi chini,Hunyamaza kimya;Wametupa mavumbi juu ya vichwa vyao,Wamejivika viunoni nguo za magunia;Wanawali wa Yerusalemu huinama vichwa vyaoKuielekea nchi.

11. Macho yangu yamechoka kwa machozi,Mtima wangu umetaabika;Ini langu linamiminwa juu ya nchiKwa uharibifu wa binti ya watu wangu;Kwa sababu watoto wachanga na wanyonyao,Huzimia katika mitaa ya mji.

12. Wao huwauliza mama zao,Zi wapi nafaka na divai?Hapo wazimiapo kama waliojeruhiwaKatika mitaa ya mji,Hapo walipomiminika nafsi zaoVifuani mwa mama zao.

13. Nikushuhudie nini? Nikufananishe na nini,Ee Binti Yerusalemu?Nikusawazishe na nini, nipate kukufariji,Ee bikira binti Sayuni?Kwa maana uvunjifu wako ni mkuu kama bahari,Ni nani awezaye kukuponya?

14. Manabii wako wameona maono kwa ajili yakoYa ubatili na upumbavuWala hawakufunua uovu wako,Wapate kurudisha kufungwa kwako;Bali wameona mabashiri ya ubatili kwa ajili yakoNa sababu za kuhamishwa.

Omb. 2