2. Kwa sababu umefanya mji kuwa ni chungu;Mji wenye boma kuwa ni magofu;Jumba la wageni kuwa si mji;Hautajengwa tena milele.
3. Kwa hiyo watu walio hodari watakutukuza,Mji wa mataifa watishao utakuogopa.
4. Maana umekuwa ngome ya maskini,Ngome ya mhitaji katika dhiki yake,Mahali pa kukimbilia wakati wa tufani,Kivuli wakati wa hari;Wakati uvumapo upepo wa watu watishao,Kama dhoruba ipigayo ukuta.
5. Kama vile hari katika mahali pakavuUtaushusha mshindo wa wageni;Kama ilivyo hari kwa kivuli cha wingu,Wimbo wa hao watishao utashushwa.
6. Na katika mlima huu BWANA wa majeshi atawafanyia mataifa yote karamu ya vitu vinono, karamu ya divai iliyokaa juu ya urojorojo wake, karamu ya vinono vilivyojaa mafuta, karamu ya divai iliyokaa juu ya urojorojo wake, iliyochujwa sana.
7. Naye katika mlima huu atauharibu uso wa sitara iliyowekwa juu ya watu wote, na utaji ule uliotandwa juu ya mataifa yote.
8. Amemeza mauti hata milele; na Bwana MUNGU atafuta machozi katika nyuso zote; na aibu ya watu wake ataiondoa katika ulimwengu wote; maana BWANA amenena hayo.
9. Katika siku hiyo watasema,Tazama, huyu ndiye Mungu wetu,Ndiye tuliyemngoja atusaidie;Huyu ndiye BWANA tuliyemngoja,Na tushangilie na kuufurahia wokovu wake.