12. Je! Si kitu kwenu, enyi nyote mpitao njia,Angalieni, mtazameKama kuna majonzi yo yote mfano wa majonzi yangu,Niliyotendwa mimi,Ambayo BWANA amenihuzunisha kwa hayoSiku ya hasira yake iwakayo.
13. Toka juu amepeleka moto mifupani mwangu,Nao umeishinda;Ametandika wavu aninase miguu,Amenirudisha nyuma;Amenifanya kuwa mtu wa pekee,Na mgonjwa mchana kutwa.
14. Kongwa la makosa yangu limefungwa na mkono wake;Hayo yameshikamana;Yamepanda juu shingoni mwangu;Amezikomesha nguvu zangu;
15. Bwana amenitia mikononi mwao,Ambao siwezi kupingamana nao.Bwana amewafanya mashujaa wangu woteKuwa si kitu kati yangu;Ameita mkutano mkuu kinyume changuIli kuwaponda vijana wangu;Bwana amemkanyaga kama shinikizoniHuyo bikira binti Yuda.
16. Mimi ninayalilia mambo hayo;Jicho langu, jicho langu linachuruzika maji;Kwa kuwa mfariji yu mbali nami,Ambaye ilimpasa kunihuisha nafsi;Watoto wangu wameachwa peke yao,Kwa sababu huyo adui ameshinda.
17. Sayuni huinyosha mikono yake;Hakuna hata mmoja wa kumfariji;BWANA ametoa amri juu ya Yakobo,Kwamba wamzungukao wawe watesi wake;Yerusalemu amekuwa kati yaoKama kitu kichafu.
18. BWANA ndiye mwenye haki;Maana nimeiasi amri yake;Sikieni, nawasihi, enyi watu wote,Mkayatazame majonzi yangu;Wasichana wangu na wavulana wanguWamechukuliwa mateka.
19. Naliwaita hao walionipendaLakini walinidanganya;Makuhani wangu na wazee wanguWalifariki mjini;Hapo walipokuwa wakitafuta chakulaili kuzihuisha nafsi zao.