5. Simeoni na Lawi ni ndugu;Panga zao ni silaha za jeuri.
6. Nafsi yangu, usiingie katika siri yao,Fahari yangu usiungane na kusanyiko lao,Maana katika ghadhabu yao walimuua mtu,Na kwa ukaidi wao walikata mshipa wa ng’ombe;
7. Ghadhabu yao na ilaaniwe, maana ilikuwa kali,Na hasira yao, maana ilikuwa haina huruma.Nitawagawa katika Yakobo,Nitawatawanya katika Israeli.
8. Yuda, ndugu zako watakusifu,Mkono wako utakuwa shingoni mwa adui zako.Wana wa baba yako watakuinamia.
9. Yuda ni mwana-simba,Kutoka katika mawindo, mwanangu, umepanda;Aliinama akajilaza kama simba,Na kama simba mke; ni nani atakaye mwamsha?
10. Fimbo ya enzi haitaondoka katika Yuda,Wala mfanya sheria kati ya miguu yake,Hata atakapokuja Yeye, mwenye milki,Ambaye mataifa watamtii.
11. Atafunga punda wake katika mzabibu,Na mwana-punda wake katika mzabibu mzuri.Amefua nguo zake kwa mvinyo,Na mavazi yake kwa damu ya zabibu.
12. Macho yake yatakuwa mekundu kwa mvinyo,Na meno yake yatakuwa meupe kwa maziwa.
13. Zabuloni atakaa pwani ya bahari,Naye atakuwa kama pwani za kuegesha merikebu,Na mpaka wake utakuwa kando ya Sidoni.
14. Isakari ni punda hodari,Ajilazaye kati ya mazizi ya kondoo;
15. Akaona mahali pa raha, kuwa pema,Na nchi, ya kuwa ni nzuri,Akainama bega lake lichukue mizigo,Akawa mtumishi kwa kazi ngumu.
16. Dani atahukumu watu wake,Kama moja ya makabila ya Israeli;
17. Dani atakuwa nyoka barabarani,Bafe katika njia,Aumaye visigino vya farasi,Hata apandaye ataanguka chali.
18. Wokovu wako nimeungoja, Ee BWANA.
19. Gadi, jeshi litamsonga,Lakini atawasonga wao mpaka visigino.
20. Asheri, chakula chake kitakuwa kinono,Naye atatoa tunu za kifalme.