Kum. 33:9-20 Swahili Union Version (SUV)

9. Aliyemtaja baba yake na mama yake, Mimi sikumwona;Wala nduguze hakuwakubali;Wala hakuwajua watoto wake mwenyewe;Maana wameliangalia neno lako,Wamelishika agano lako.

10. Watamfundisha Yakobo hukumu zako,Na Israeli torati yako,Wataweka uvumba mbele zako,Na sadaka nzima za kuteketezwa madhabahuni mwako.

11. Ee BWANA, ubariki mali zake,Utakabali kazi ya mikono yake;Uwapige viuno vyao waondokao juu yake,Na wenye kumchukia, wasiinuke tena.

12. Akamnena Benyamini,Mpenzi wa BWANA atakaa salama kwake;Yuamfunika mchana kutwa,Naye hukaa kati ya mabega yake.

13. Na Yusufu akamnena,Nchi yake na ibarikiwe na BWANA;Kwa vitu vya thamani vya mbinguni, kwa huo umande,Na kwa kilindi kilalacho chini,

14. Na kwa vitu vilivyo bora vya matunda ya jua,Na kwa vitu vilivyo bora vya maongeo ya miezi,

15. Na kwa vitu viteule vya milima ya kale,Na kwa vitu vilivyo bora vya vilima vya milele,

16. Na kwa vitu vilivyo bora vya nchi, na kujaa kwake,Na uradhi wake aliyekaa ndani ya kile kijiti;Na ije baraka juu ya kichwa chake Yusufu,Juu ya utosi wa kichwa chake aliyetengwa na nduguze.

17. Mzaliwa wa kwanza wa ng’ombe wake mume, enzi ni yake;Na pembe zake ni pembe za nyati;Kwa hizo atayasukuma mataifa yote, hata ncha za nchi;Nao ni makumi ya maelfu ya Efraimu,Nao ni maelfu ya Manase.

18. Na Zabuloni akamnena,Furahi Zabuloni, katika kutoka kwako;Na Isakari, katika hema zako.

19. Watayaita mataifa waje mlimani;Wakasongeze huko sadaka za haki;Kwa kuwa watanyonya wingi wa bahari,Na akiba zilizofichamana za mchangani.

20. Na Gadi akamnena,Na abarikiwe amwongezaye Gadi;Yeye hukaa kama simba mke,Hurarua mkono, naam, na utosi wa kichwa.

Kum. 33