13. Kwa sababu hiyo watu wangu wamechukuliwa mateka, kwa kukosa kuwa na maarifa; na watu wao wenye cheo wana njaa, na wengi wao waona kiu sana.
14. Kwa hiyo kuzimu kumeongeza tamaa yake, kumefunua kinywa chake bila kiasi; na utukufu wao, na wingi wao, na ghasia yao, naye pia afurahiye miongoni mwao, hushuka na kuingia humo.
15. Na mtu mnyonge ainamishwa, na mtu mkubwa amedhilika, na macho yao walioinuka hunyenyekezwa,
16. bali BWANA wa majeshi ametukuzwa katika hukumu, na Mungu aliye Mtakatifu ametakaswa katika haki.
17. Ndipo wana-kondoo watakapolisha kama katika malisho yao wenyewe, na mahali pao waliowanda, palipoachwa ukiwa, wageni watakula.
18. Ole wao wavutao uovu kwa kamba za ubatili, na dhambi kama kwa kamba za gari!
19. Wasema, Na afanye haraka, aihimize kazi yake, tupate kuiona; na likaribie shauri lake aliye Mtakatifu wa Israeli, tupate kuliona.
20. Ole wao wasemao kwamba uovu ni wema, na kwamba wema ni uovu; watiao giza badala ya nuru, na nuru badala ya giza; watiao uchungu badala ya utamu, na utamu badala ya uchungu!
21. Ole wao walio wenye hekima katika macho yao wenyewe, na wenye busara katika fikira zao wenyewe!
22. Ole wao walio hodari kunywa kileo chenye nguvu, watu waume wenye nguvu kuchanganya vileo;
23. wampao haki mwenye uovu, ili wapewe ijara, na kumwondolea mwenye haki haki yake!
24. Kwa hiyo kama vile mwali wa moto uteketezavyo mabua makavu, na kama manyasi makavu yaangukavyo katika mwali wa moto; kadhalika shina lao litakuwa kama ubovu, na ua lao litapeperushwa juu kama mavumbi; kwa sababu wameikataa sheria ya BWANA wa majeshi, na kulidharau neno lake aliye Mtakatifu wa Israeli.
25. Kwa sababu hiyo hasira ya BWANA imewaka juu ya watu wake, naye amenyosha mkono wake juu yao; akawapiga, navyo vilima vilitetemeka, na mizoga yao ilikuwa kama takataka katika njia kuu. Pamoja na hayo yote hasira yake haikugeukia mbali, lakini mkono wake umenyoshwa hata sasa.
26. Naye atawatwekea bendera mataifa toka mbali,Naye atawapigia miunzi tokea mwisho wa nchi;Na tazama, watakuja mbio mbio upesi sana.
27. Miongoni mwao hakuna achokaye wala kukwaa;Hakuna asinziaye wala kulala usingizi;Wala mshipi wa viuno vyao hautalegea.Wala ukanda wa viatu vyao hautakatika;
28. Mishale yao ni mikali, na pindi zao zote zimepindika;Kwato za farasi zao zitahesabika kama gumegume;Na gurudumu zao kama kisulisuli;
29. Ngurumo yao itakuwa kama ya simba;Watanguruma kama wana-simba;Naam, watanguruma na kukamata mateka,Na kuyachukua na kwenda zao salama,Wala hakuna mtu atakayeokoa.
30. Nao watanguruma juu yao siku hiyoKama ngurumo ya bahari;Na mtu akiitazama nchi, ataona giza na dhikiNayo nuru imetiwa giza katika mawingu yake.