10. Mimi nalikuwa ukuta,Na maziwa yangu kama minara;Ndipo nikawa machoni pakeKama mtu aliyeipata amani.
11. Sulemani alikuwa na shamba la mizabibu huko Baal-hamomiAkawakodisha walinzi hilo shamba lake la mizabibu;Kila mtu atoe vipande elfu vya fedha kwa matunda yake.
12. Shamba langu la mizabibu, lililo langu mimi, li mbele yangu.Basi, Sulemani, wewe uwe na elfu zako,Na hao wayalindao matunda yake wapewe mia mbili.
13. Wewe ukaaye bustanini,Hao rafiki huisikiliza sauti yako;Unisikizishe mimi.
14. Ukimbie, mpendwa wangu,Nawe uwe kama paa, au ayala,Juu ya milima ya manukato.