Wim. 5:10-15 Swahili Union Version (SUV)

10. Mpendwa wangu ni mweupe, tena mwekundu,Mashuhuri miongoni mwa elfu kumi;

11. Kichwa chake ni kama dhahabu safi sana,Nywele zake ni za ukoka, nyeusi kama kunguru;

12. Macho yake ni kama hua penye vijito,Wakioga kwa maziwa, wakiikalia mito iliyojaa;

13. Mashavu yake ni kama matuta ya rihani,Ambayo hufanyizwa manukato;Midomo yake ni kama nyinyoro,Inadondoza matone ya manemane;

14. Mikono yake ni kama mianzi ya dhahabu,lliyopambwa kwa zabarajadi;Kiwiliwili chake kama kazi ya pembe,Iliyonakishiwa kwa yakuti samawi;

15. Miguu yake ni kama nguzo za marimari,Zilizowekwa juu ya misingi ya dhahabu;Sura yake ni kama Lebanoni,Ni bora mfano wa mierezi;

Wim. 5