7. Siku za mateso na misiba yake,Yerusalemu huyakumbuka matamaniko yake yoteYaliyokuwa tangu siku za kale;Hapo watu wake walipoanguka mikononi mwa mtesi,Wala hakuna hata mmoja wa kumsaidia;Hao watesi wake walimwona,Wakafanya sabato zake kuwa mzaha.
8. Yerusalemu amefanya dhambi sana;Kwa hiyo amekuwa kama kitu kichafu;Wote waliomheshimu wanamdharau,Kwa sababu wameuona uchi wake;Naam, yeye anaugua,Na kujigeuza aende nyuma.
9. Uchafu wake ulikuwa katika marinda yake;Hakukumbuka mwisho wake;Kwa hiyo ameshuka kwa ajabu;Yeye hana mtu wa kumfariji;Tazama, BWANA, teso langu;Maana huyo adui amejitukuza.
10. Huyo mtesi amenyosha mkono wakeJuu ya matamaniko yake yote;Maana ameona ya kuwa makafiri wameingiaNdani ya patakatifu pake;Ambao kwa habari zao wewe uliamuruWasiingie katika kusanyiko lako.
11. Watu wake wote hupiga kite,Wanatafuta chakula;Wameyatoa matamaniko yao wapate chakulaCha kuihuisha nafsi;Ee BWANA, tazama, uangalie;Kwa maana mimi nimekuwa mnyonge.
12. Je! Si kitu kwenu, enyi nyote mpitao njia,Angalieni, mtazameKama kuna majonzi yo yote mfano wa majonzi yangu,Niliyotendwa mimi,Ambayo BWANA amenihuzunisha kwa hayoSiku ya hasira yake iwakayo.
13. Toka juu amepeleka moto mifupani mwangu,Nao umeishinda;Ametandika wavu aninase miguu,Amenirudisha nyuma;Amenifanya kuwa mtu wa pekee,Na mgonjwa mchana kutwa.
14. Kongwa la makosa yangu limefungwa na mkono wake;Hayo yameshikamana;Yamepanda juu shingoni mwangu;Amezikomesha nguvu zangu;
15. Bwana amenitia mikononi mwao,Ambao siwezi kupingamana nao.Bwana amewafanya mashujaa wangu woteKuwa si kitu kati yangu;Ameita mkutano mkuu kinyume changuIli kuwaponda vijana wangu;Bwana amemkanyaga kama shinikizoniHuyo bikira binti Yuda.