17. Walitoa sadaka kwa pepo, si Mungu,Kwa miungu wasiyoijua,Kwa miungu mipya iliyotokea siku zilizo karibu,Ambayo baba zenu hawakuiogopa.
18. Humkumbuki Mwamba aliyekuzaa,Mungu aliyekuzaa umemsahau.
19. BWANA akaona, akawachukia,Kwa sababu ya kukasirishwa na wanawe na binti zake.
20. Akasema, Nitawaficha uso wangu,Nitaona mwisho wao utakuwaje;Maana, ni kizazi cha ukaidi mwingi,Watoto wasio imani ndani yao.
21. Wamenitia wivu kwa kisicho Mungu;Wamenikasirisha kwa ubatili wao;Nami nitawatia wivu kwa wasio watu,Nami nitawakasirisha kwa taifa lipumbaalo.
22. Maana, moto umewashwa kwa hasira yangu,Unateketea hata chini ya kuzimu,Unakula dunia pamoja na mazao yake,Unaunguza misingi ya milima.
23. Nitaweka madhara juu yao chunguchungu;Nitawapiga kwa mishale yangu hata ikaishe;
24. Watakonda kwa njaa, wataliwa na makaa ya moto,Na uharibifu mkali;Nitawapelekea meno ya wanyama wakali,Pamoja na sumu ya wadudu watambaao mavumbini.
25. Nje upanga utawafifilizaNa ndani ya vyumba, utisho;Utaangamiza mvulana na msichana,Anyonyaye pamoja na mwenye mvi,
26. Nalisema, Ningewatawanyia mbali,Ningekomesha kumbukumbu lao kati ya wanadamu;
27. Isipokuwa naliogopa makamio ya adui,Adui zao wasije wakafikiri uongo,Wasije wakasema, Mkono wetu umetukuka,Wala BWANA hakuyafanya haya yote.
28. Maana hawa ni taifa wasio shauri,Wala fahamu hamna ndani yao.
29. Laiti wangekuwa na akili, hata wakafahamu haya,Ili watafakari mwisho wao.
30. Mmoja angefukuzaje watu elfu,Wawili wangekimbizaje elfu kumi,Kama Mwamba wao asingaliwauza,Kama BWANA asingaliwatoa?
31. Maana, Mwamba wao si kama Mwamba wetu,Hata adui zetu wenyewe ndivyo wahukumuvyo.
32. Maana, mzabibu wao ni mzabibu wa Sodoma,Nao ni wa mashamba ya Gomora;Zabibu zao ni zabibu za uchungu,Vichala vyao ni vichungu.
33. Mvinyo yao ni sumu ya majoka,Uchungu mkali wa nyoka.
34. Je! Haya hayakuwekwa akiba kwangu?Na kutiwa muhuri kati ya hazina yangu?