22. Dunia iliumbwa na huyo aketiye juu ya mbingu;kutoka huko wakazi wa dunia ni kama panzi!Yeye amezitandaza mbingu kama pazia,na kuzikunjua kama hema la kuishi.
23. Yeye huwaporomosha wakuu wenye nguvu,watawala wa dunia huwafanya kuwa si kitu.
24. Mara tu wanaposimikwa na kuanza kuota,hata kabla hawajatoa mizizi kama miti udongoni,Mwenyezi-Mungu akiwapulizia hunyauka,kimbunga huwapeperusha kama makapi!