Zab. 78:7-13 Swahili Union Version (SUV)

7. Wamwekee Mungu tumaini lao.Wala wasiyasahau matendo ya Mungu,Bali wazishike amri zake.

8. Naam, wasiwe kama baba zao,Kizazi cha ukaidi na uasi.Kizazi kisichojitengeneza moyo,Wala roho yake haikuwa amini kwa Mungu.

9. Wale Waefraimu, wenye silaha, wapiga upinde,Walirudi nyuma siku ya vita.

10. Hawakulishika agano la Mungu;Wakakataa kuenenda katika sheria yake;

11. Wakayasahau matendo yake,Na mambo yake ya ajabu aliyowaonyesha.

12. Mbele ya baba zao alifanya mambo ya ajabu,Katika nchi ya Misri, konde la Soani.

13. Aliipasua bahari akawavusha;Aliyasimamisha maji mfano wa chungu.

Zab. 78