5. Maana mautini hapana kumbukumbu lako;Katika kuzimu ni nani atakayekushukuru?
6. Nimechoka kwa kuugua kwangu;Kila usiku nakieleza kitanda changu;Nalilowesha godoro langu kwa machozi yangu.
7. Jicho langu limeharibika kwa masumbufu,Na kuchakaa kwa sababu yao wanaoniudhi.
8. Ondokeni kwangu, ninyi nyote mtendao uovu;Kwa kuwa BWANA ameisikia sauti ya kilio changu.
9. BWANA ameisikia dua yangu;BWANA atayatakabali maombi yangu.