Zab. 6:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. BWANA, usinikemee kwa hasira yako,Wala usinirudi kwa ghadhabu yako.

2. BWANA, unifadhili, maana ninanyauka;BWANA, uniponye, mifupa yangu imefadhaika.

3. Na nafsi yangu imefadhaika sana;Na Wewe, BWANA, hata lini?

4. BWANA urudi, uniopoe nafsi yangu,Uniokoe kwa ajili ya fadhili zako.

5. Maana mautini hapana kumbukumbu lako;Katika kuzimu ni nani atakayekushukuru?

Zab. 6