7. Tazama, kwa vinywa vyao huteuka,Midomoni mwao mna panga,Kwa maana ni nani asikiaye?
8. Na Wewe, BWANA, utawacheka,Utawadhihaki mataifa yote.
9. Ee nguvu zangu, nitakungoja Wewe,Maana Mungu ndiye aliye ngome yangu
10. Mungu wa fadhili zangu atanitangulia,Mungu atanijalia kuwatazama adui zangu.
11. Usiwaue, watu wangu wasije wakasahau;Uwatawanye kwa uweza wako,Na kuwaangamiza, Ee Bwana, ngao yetu.
12. Kwa dhambi ya kinywa chao,Na kwa neno la midomo yao,Wanaswe kwa kiburi chao,Kwa ajili ya kulaani na uongo wasemao.
13. Uwakomeshe kwa hasira,Uwakomeshe watoweke,Wajue ya kuwa Mungu atawala katika Yakobo,Na hata miisho ya dunia.
14. Wakati wa jioni hurudi, hulia kama mbwa,Na kuzunguka-zunguka mjini.