3. Maana si kwa upanga wao walivyoimiliki nchi,Wala si mkono wao uliowaokoa;Bali mkono wako wa kuume, naam, mkono wako,Na nuru ya uso wako, kwa kuwa uliwaridhia.
4. Ee Mungu, Wewe ndiwe mfalme wangu,Uagize mambo ya wokovu kwa Yakobo.
5. Kwa nguvu zako tutawaangusha watesi wetu;Kwa jina lako tutawakanyaga watupingao.