7. Maana bila sababu wamenifichia wavu,Bila sababu wameichimbia shimo nafsi yangu.
8. Uharibifu na umpate kwa ghafula,Na wavu aliouficha umnase yeye mwenyewe;Kwa uharibifu aanguke ndani yake.
9. Na nafsi yangu itamfurahia BWANA,Na kuushangilia wokovu wake.
10. Mifupa yangu yote itasema,BWANA, ni nani aliye kama Wewe?Umponyaye maskini na mtu aliye hodari kumshinda yeye,Naam, maskini na mhitaji na mtu amtekaye.
11. Mashahidi wa udhalimu wanasimama,Wananiuliza mambo nisiyoyajua.
12. Wananilipa mabaya badala ya mema,Hata nafsi yangu ikaingia ukiwa.
13. Bali mimi, walipougua wao,Nguo yangu ilikuwa gunia.Nalijitesa nafsi yangu kwa kufunga;Maombi yangu yakarejea kifuani mwangu.
14. Nalijifanya kama kwamba ni rafiki au ndugu yangu,Naliinama nikilia kama aliyefiwa na mamaye.
15. Lakini nikijikwaa hufurahi na kukusanyana,Walinikusanyikia watu ovyo nisiowajua,Wananipapura wala hawakomi.
16. Kama wenye mzaha wakikufuru karamuniWananisagia meno.
17. BWANA, hata lini utatazama?Uiokoe nafsi yangu na maharabu yao,Na mpenzi wangu na wana-simba.
18. Nitakushukuru katika kusanyiko kubwa;Nitakusifu kati ya watu wengi.