23. Uamke, uwe macho ili kunipatia hukumuKwa ajili ya madai yangu,Mungu wangu na Bwana wangu.
24. Unihukumu kwa haki yako,Ee BWANA, Mungu wangu,Wala wasinisimangize.
25. Wasiseme moyoni, Haya! Ndivyo tutakavyo;Wasiseme, Tumemmeza.
26. Waaibishwe, wafedheheshwe pamoja,Wanaoifurahia hali yangu mbaya.Wavikwe aibu na fedheha,Wanaojikuza juu yangu.
27. Washangilie na kufurahi,Wapendezwao na haki yangu.Naam, waseme daima, Atukuzwe BWANA,Apendezwaye na amani ya mtumishi wake.