Zab. 32:1-6 Swahili Union Version (SUV)

1. Heri aliyesamehewa dhambi,Na kusitiriwa makosa yake.

2. Heri BWANA asiyemhesabia upotovu,Ambaye rohoni mwake hamna hila.

3. Niliponyamaza mifupa yangu ilichakaaKwa kuugua kwangu mchana kutwa.

4. Kwa maana mchana na usikuMkono wako ulinilemea.Jasho langu likakauka hata nikawaKama nchi kavu wakati wa kaskazi.

5. Nalikujulisha dhambi yangu,Wala sikuuficha upotovu wangu.Nalisema, Nitayakiri maasi yangu kwa BWANA,Nawe ukanisamehe upotovu wa dhambi yangu.

6. Kwa hiyo kila mtu mtauwaAkuombe wakati unapopatikana.Hakika maji makuu yafurikapo,Hayatamfikia yeye.

Zab. 32