1. Ee BWANA, nitakutukuza kwa maana umeniinua,Wala hukuwafurahisha adui zangu juu yangu.
2. Ee BWANA, Mungu wangu,Nalikulilia ukaniponya.
3. Umeniinua nafsi yangu,Ee BWANA, kutoka kuzimu.Umenihuisha na kunitoaMiongoni mwao washukao shimoni.
4. Mwimbieni BWANA zaburi,Enyi watauwa wake.Na kufanya shukrani.Kwa kumbukumbu la utakatifu wake.