Zab. 25:16-20 Swahili Union Version (SUV)

16. Uniangalie na kunifadhili,Maana mimi ni mkiwa na mteswa.

17. Katika shida za moyo wangu unifanyie nafasi,Na kunitoa katika dhiki zangu.

18. Utazame teso langu na taabu yangu;Unisamehe dhambi zangu zote.

19. Uwatazame adui zangu, maana ni wengi,Wananichukia kwa machukio ya ukali.

20. Unilinde nafsi yangu na kuniponya,Nisiaibike, maana nakukimbilia Wewe.

Zab. 25