5. Heri atendaye fadhili na kukopesha;Atengenezaye mambo yake kwa haki.
6. Kwa maana hataondoshwa kamwe;Mwenye haki atakumbukwa milele.
7. Hataogopa habari mbaya;Moyo wake u imara ukimtumaini BWANA.
8. Moyo wake umethibitika hataogopa,Hata awaone watesi wake wameshindwa.
9. Amekirimu, na kuwapa maskini,Haki yake yakaa milele,Pembe yake itatukuzwa kwa utukufu.