Zab. 112:1-8 Swahili Union Version (SUV)

1. Haleluya.Heri mtu yule amchaye BWANA,Apendezwaye sana na maagizo yake.

2. Wazao wake watakuwa hodari duniani;Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa.

3. Nyumbani mwake mna utajiri na mali,Na haki yake yakaa milele.

4. Nuru huwazukia wenye adili gizani;Ana fadhili na huruma na haki.

5. Heri atendaye fadhili na kukopesha;Atengenezaye mambo yake kwa haki.

6. Kwa maana hataondoshwa kamwe;Mwenye haki atakumbukwa milele.

7. Hataogopa habari mbaya;Moyo wake u imara ukimtumaini BWANA.

8. Moyo wake umethibitika hataogopa,Hata awaone watesi wake wameshindwa.

Zab. 112