Zab. 101:4-7 Swahili Union Version (SUV)

4. Moyo wa ukaidi utaondoka kwangu,Lililo ovu sitalijua.

5. Amsingiziaye jirani yake kwa siri,Huyo nitamharibu.Mwenye macho ya kiburi na moyo wa majivuno,Huyo sitavumilia naye.

6. Macho yangu yatawaelekea waaminifu katika nchi,Hao wakae nami.Yeye aendaye katika njia kamilifu,Ndiye atakayenitumikia.

7. Hatakaa ndani ya nyumba yanguMtu atendaye hila.Asemaye uongo hatathibitikaMbele ya macho yangu.

Zab. 101