1. Ndipo Yona akamwomba BWANA, Mungu wake, katika tumbo la yule samaki,
2. Akasema,Nalimlilia BWANA kwa sababu ya shida yangu,Naye akaniitikia;Katika tumbo la kuzimu naliomba,Nawe ukasikia sauti yangu.
3. Maana ulinitupa vilindini,Ndani ya moyo wa bahari;Gharika ya maji ikanizunguka pande zote;Mawimbi yako yote na gharika zako zote zimepita juu yangu.
4. Nami nikasema, Nimetupwa mbali na macho yako;Lakini nitatazama tena kukabili hekalu lako takatifu.