Yer. 9:21-26 Swahili Union Version (SUV)

21. Kwa maana mauti imepandia madirishani mwetu,imeingia majumbani mwetu;Ipate kuwakatilia mbali watoto walio nje,na vijana katika njia kuu.

22. Nena, BWANA asema hivi,Mizoga ya watu itaangukakama samadi juu ya mashamba,Na kama konzi ya ngano nyuma yake avunaye,wala hapana mtu atakayeikusanya.

23. BWANA asema hivi, Mwenye hekima asijisifu kwa sababu ya hekima yake, wala mwenye nguvu asijisifu kwa sababu ya nguvu zake, wala tajiri asijisifu kwa sababu ya utajiri wake;

24. bali ajisifuye na ajisifu kwa sababu hii, ya kwamba ananifahamu mimi, na kunijua, ya kuwa mimi ni BWANA, nitendaye wema, na hukumu, na haki, katika nchi; maana mimi napendezwa na mambo hayo, asema BWANA,

25. Tazama, siku zinakuja, asema BWANA, nitakapowaadhibu wote waliotahiriwa katika hali yao ya kutokutahiriwa;

26. Misri, na Yuda, na Edomu, na wana wa Amoni, na Moabu, na wote wenye kunyoa denge, wakaao nyikani; maana mataifa hayo yote hawana tohara, wala nyumba yote ya Israeli hawakutahiriwa mioyo yao.

Yer. 9