Yer. 51:30-41 Swahili Union Version (SUV)

30. Mashujaa wa Babeli wameacha kupigana;Wanakaa katika ngome zao;Ushujaa wao umewapungukia;Wamekuwa kama wanawake;Makao yake yameteketea;Makomeo yake yamevunjika.

31. Tarishi mmoja atapiga mbio kumlaki mwingine,Na mjumbe mmoja atapiga mbio kumlaki mwenziwe,Ili kumpasha habari mfalme wa Babeli,Ya kuwa mji wake umetwaliwa kila upande.

32. Navyo vivuko vimeshambuliwa,Nayo makangaga wameyatia moto,Nao watu wa vita wameingiwa na hofu.

33. Kwa maana BWANA wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi; Binti Babeli amekuwa kama sakafu ya kufikichia wakati wa kukanyagwa kwake; bado kitambo kidogo na wakati wa mavuno utafika kwake.

34. Nebukadreza, mfalme wa Babeli, amenila, ameniseta, amenifanya kuwa chombo kitupu; amenimeza kama joka, amelijaza tumbo lake vitu vyangu vya anasa; amenitupa

35. Udhalimu niliotendwa mimi, na uliotendwa mwili wangu, umpate Babeli; ndivyo atakavyosema yeye akaaye Sayuni; na Yerusalemu atasema, Damu yangu na iwe juu yao wakaao katika Ukaldayo.

36. Basi, BWANA asema hivi, Tazama, nitakutetea, nami nitatwaa kisasi kwa ajili yako; nami nitaikausha bahari yake, nitaifanya chemchemi yake kuwa pakavu.

37. Na Babeli utakuwa magofu, makao ya mbwa-mwitu, ajabu, na mazomeo, pasipo mtu wa kukaa huko.

38. Watanguruma pamoja kama wana-simba; watanguruma kama simba wachanga.

39. Wakiingiwa na ukali, nitawafanyizia karamu yao, nami nitawalevya, wapate kufurahi, na kulala usingizi wa milele, wasiamke tena, asema BWANA.

40. Nitawatelemsha kama wana-kondoo machinjoni, kama kondoo waume pamoja na mabeberu.

41. Jinsi Sheshaki alivyotwaliwa!Naye sifa ya dunia yote alivyoshambuliwa!Jinsi Babeli alivyokuwa ukiwaKatikati ya mataifa!

Yer. 51