30. Mashujaa wa Babeli wameacha kupigana;Wanakaa katika ngome zao;Ushujaa wao umewapungukia;Wamekuwa kama wanawake;Makao yake yameteketea;Makomeo yake yamevunjika.
31. Tarishi mmoja atapiga mbio kumlaki mwingine,Na mjumbe mmoja atapiga mbio kumlaki mwenziwe,Ili kumpasha habari mfalme wa Babeli,Ya kuwa mji wake umetwaliwa kila upande.
32. Navyo vivuko vimeshambuliwa,Nayo makangaga wameyatia moto,Nao watu wa vita wameingiwa na hofu.
33. Kwa maana BWANA wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi; Binti Babeli amekuwa kama sakafu ya kufikichia wakati wa kukanyagwa kwake; bado kitambo kidogo na wakati wa mavuno utafika kwake.