12. bali katika mahali pale walipomchukua mateka ndipo atakapokufa, wala hataiona nchi hii tena kamwe.
13. Ole wake aijengaye nyumba yake kwa uovu!Na vyumba vyake kwa udhalimu!Atumiaye utumishi wa mwenzake bila ujira,Wala hampi mshahara wake;
14. Asemaye, Nitajijengea nyumba pana na vyumba vipana;Naye hujikatia madirisha;Na kuta zake zimefunikwa kwa mierezi,Na kupakwa rangi nyekundu.
15. Je! Utatawala kwa sababu unashindana na watu kwa mierezi? Baba yako, je! Hakula na kunywa, na kufanya hukumu na haki? Hapo ndipo alipofanikiwa.
16. Alihukumu maneno ya maskini na mhitaji; hapo ndipo alipofanikiwa. Je! Huku siko kunijua, asema BWANA?