14. Imba, Ee binti Sayuni; piga kelele, Ee Israeli;Furahi na kushangilia kwa moyo wako wote, Ee binti Yerusalemu.
15. BWANA ameziondoa hukumu zako,Amemtupa nje adui yako;Mfalme wa Israeli, naam, yeye BWANA, yu katikati yako;Hutaogopa uovu tena.
16. Katika siku ile Yerusalemu utaambiwa,Usiogope, Ee Sayuni; mikono yako isilegee.
17. BWANA, Mungu wako, yu katikati yako shujaa awezaye kuokoa;Atakushangilia kwa furaha kuu,Atakutuliza katika upendo wake,Atakufurahia kwa kuimba.