5. Wale waliokula vitu vya anasaWameachwa peke yao njiani;Wale waliokuzwa kuvaa nguo nyekunduWakumbatia jaa.
6. Maana uovu wa binti ya watu wangu ni mkubwaKuliko dhambi ya Sodoma,Uliopinduliwa kama katika dakika moja,Wala mikono haikuwekwa juu yake.
7. Wakuu wake walikuwa safi kuliko theluji,Walikuwa weupe kuliko maziwa;Miili yao, walikuwa wekundu kuliko marijani,Na umbo lao kama yakuti samawi.
8. Nyuso zao ni nyeusi kuliko makaa;Hawajulikani katika njia kuu;Ngozi yao yagandamana na mifupa yaoImekauka, imekuwa kama mti.
9. Heri wale waliouawa kwa upangaKuliko wao waliouawa kwa njaa;Maana hao husinyaa, wakichomwaKwa kukosa matunda ya mashamba.
10. Mikono ya wanawake wenye hurumaImewatokosa watoto wao wenyewe;Walikuwa ndio chakula chaoKatika uharibifu wa binti ya watu wangu.
11. BWANA ameitimiza kani yake,Ameimimina hasira yake kali;Naye amewasha moto katika SayuniUlioiteketeza misingi yake.
12. Wafalme wa dunia hawakusadiki,Wala wote wakaao duniani,Ya kwamba mtesi na adui wangeingiaKatika malango ya Yerusalemu.
13. Ni kwa sababu ya dhambi za manabii wakeNa maovu ya makuhani wake,Walioimwaga damu ya wenye hakiKatikati yake.
14. Hutanga-tanga njiani kama vipofu,Wametiwa unajisi kwa damu;Hata ikawa watu wasiwezeKuyagusa mavazi yao.
15. Watu waliwapigia kelele, Ondokeni, Uchafu,Ondokeni, ondokeni, msiguse;Walipokimbia na kutanga-tanga, watu walisema kati ya mataifa,Hawatakaa hapa tena.