1. Jinsi dhahabu ilivyoacha kung’aa,Na dhahabu iliyo safi ilivyobadilika!Mawe ya patakatifu yametupwaMwanzo wa kila njia.
2. Wana wa Sayuni wenye thamani,Walinganao na dhahabu safi,Jinsi wanavyodhaniwa kuwa vyombo vya udongo,Kazi ya mikono ya mfinyanzi!
3. Hata mbwa-mwitu hutoa matiti,Huwanyonyesha watoto wao;Binti ya watu wangu amekuwa mkali,Mfano wa mbuni jangwani.
4. Ulimi wa mtoto anyonyayeWagandamana na kaakaa lake kwa kiu;Watoto wachanga waomba chakula,Wala hakuna hata mmoja awamegeaye.
5. Wale waliokula vitu vya anasaWameachwa peke yao njiani;Wale waliokuzwa kuvaa nguo nyekunduWakumbatia jaa.
6. Maana uovu wa binti ya watu wangu ni mkubwaKuliko dhambi ya Sodoma,Uliopinduliwa kama katika dakika moja,Wala mikono haikuwekwa juu yake.
7. Wakuu wake walikuwa safi kuliko theluji,Walikuwa weupe kuliko maziwa;Miili yao, walikuwa wekundu kuliko marijani,Na umbo lao kama yakuti samawi.
8. Nyuso zao ni nyeusi kuliko makaa;Hawajulikani katika njia kuu;Ngozi yao yagandamana na mifupa yaoImekauka, imekuwa kama mti.