19. Ndivyo zilivyo njia za kila mwenye tamaa ya mali;Huuondoa uhai wao walio nayo.
20. Hekima hupaza sauti yake katika njia kuu,Hutoa sauti yake katika viwanja;
21. Hulia penye mikutano mikubwa ya watu,Mahali pa kuyaingilia malango,Ndani ya mji hutamka maneno yake.
22. Enyi wajinga, hata lini mtapenda ujinga?Na wenye dharau kupenda dharau yao,Na wapumbavu kuchukia maarifa?
23. Geukeni kwa ajili ya maonyo yangu;Tazama, nitawamwagia roho yangu,Na kuwajulisheni maneno yangu.
24. Kwa kuwa nimeita, nanyi mkakataa;Nimeunyosha mkono wangu, asiangalie mtu;
25. Bali mmebatilisha shauri langu,Wala hamkutaka maonyo yangu;
26. Mimi nami nitacheka siku ya msiba wenu,Nitadhihaki hofu yenu ifikapo;
27. Hofu yenu ifikapo kama tufani,Na msiba wenu ufikapo kama kisulisuli,Dhiki na taabu zitakapowafikia.
28. Ndipo watakaponiita, lakini sitaitika;Watanitafuta kwa bidii, wasinione.
29. Kwa kuwa walichukia maarifa,Wala hawakuchagua kumcha BWANA.
30. Hawakukubali mashauri yangu,Wakayadharau maonyo yangu yote.
31. Kwa hiyo watakula matunda ya njia yao,Watashiba mashauri yao wenyewe.
32. Maana kurudi nyuma kwao wajinga kutawaua,Na kufanikiwa kwao wapumbavu kutawaangamiza.