Mhu. 9:16-18 Swahili Union Version (SUV)

16. Ndipo niliposema, Bora hekima kuliko nguvu; walakini hekima ya maskini hudharauliwa, wala maneno yake hayasikilizwi.

17. Maneno ya wenye hekima yanenwayo taratibu husikiwa,Zaidi ya mlio wake atawalaye katikati ya wapumbavu.

18. Hekima ndiyo bora kupita silaha za vita;Lakini mkosaji mmoja huharibu mema mengi.

Mhu. 9