15. Basi, kulionekana humo mtu maskini mwenye hekima, naye kwa hekima yake akauokoa mji ule lakini hata hivyo hapakuwa na mtu ye yote aliyemkumbuka yule mtu maskini.
16. Ndipo niliposema, Bora hekima kuliko nguvu; walakini hekima ya maskini hudharauliwa, wala maneno yake hayasikilizwi.
17. Maneno ya wenye hekima yanenwayo taratibu husikiwa,Zaidi ya mlio wake atawalaye katikati ya wapumbavu.
18. Hekima ndiyo bora kupita silaha za vita;Lakini mkosaji mmoja huharibu mema mengi.