1. Mainzi mafu huvundisha marhamu ya mwuza marashi;Kadhalika upumbavu haba ni mzito kuliko hekima na heshima.
2. Moyo wake mwenye hekima upo upande wa kuume;Bali moyo wake mpumbavu upo mkono wa kushoto.
3. Naam, huyo mpumbavu tena, aendapo njiani, hupungukiwa na fahamu zake; hata humwambia kila mtu ya kuwa yeye ni mpumbavu.
4. Roho yake mtawala ikiinuka kinyume chako,Usiondoke mara mahali pako ulipo;Kwa maana roho ya upole hutuliza machukizo yaliyo makubwa.
5. Liko baa nililoliona chini ya jua, nalo ni kama kosa litokalo kwake yeye atawalaye;
6. ya kuwa upumbavu huwekwa mahali pa juu sana, nao wakwasi hukaa mahali pa chini.
7. Mimi nimeona watumwa wamepanda farasi, na wakuu wakienda kwa miguu juu ya nchi kama watumwa.
8. Mwenye kuchimba shimo atatumbukia ndani yake;Na yeye abomoaye boma, nyoka atamwuma.
9. Mwenye kuchonga mawe ataumizwa kwayo;Naye apasuaye miti huona hatari katika hiyo.