Lk. 20:14-27 Swahili Union Version (SUV)

14. Lakini, wale wakulima walipomwona, walishauriana wao kwa wao, wakisema, Huyu ndiye mrithi; haya, na tumwue, ili urithi uwe wetu.

15. Wakamtupa nje ya shamba la mizabibu, wakamwua. Basi, bwana wa shamba la mizabibu atawatendeje?

16. Atakuja na kuwaangamiza wakulima wale, na lile shamba la mizabibu atawapa wengine. Waliposikia hayo walisema, Hasha! Yasitukie haya!

17. Akawakazia macho akasema, Maana yake nini basi neno hili lililoandikwa,Jiwe walilolikataa waashi,Hilo limekuwa jiwe kuu la pembeni?

18. Kila mtu aangukaye juu ya jiwe hilo atavunjika-vunjika; na ye yote ambaye litamwangukia litamsaga kabisa.

19. Nao waandishi na wakuu wa makuhani walitafuta kumkamata saa iyo hiyo, wakawaogopa watu, maana walitambua ya kwamba mfano huu amewanenea wao.

20. Wakamvizia-vizia, wakatuma wapelelezi waliojifanya kuwa watu wa haki, ili wamnase katika maneno yake, wapate kumtia katika enzi na mamlaka ya liwali.

21. Wakamwuliza, wakisema, Mwalimu, twajua ya kwamba wasema na kufundisha yaliyo ya haki, wala hujali cheo cha mtu, bali unafundisha njia ya Mungu kwa kweli.

22. Je! Ni halali tumpe Kaisari kodi, au sivyo?

23. Lakini yeye alitambua hila yao, akawaambia,

24. Nionyesheni dinari. Ina sura na anwani ya nani? Wakamjibu, Ya Kaisari.

25. Akawaambia, Basi, vya Kaisari mpeni Kaisari, na vya Mungu mpeni Mungu.

26. Wala hawakuweza kumshitaki kwa maneno yake mbele ya watu; wakastaajabia majibu yake, wakanyamaa.

27. Kisha baadhi ya Masadukayo wakamwendea, wale wasemao ya kwamba hakuna ufufuo, wakamwuliza,

Lk. 20