42. Bwana akasema, Ni nani, basi, aliye wakili mwaminifu, mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya utumishi wake wote, awape watu posho kwa wakati wake?
43. Heri mtumwa yule, ambaye bwana wake ajapo atamkuta anafanya hivyo.
44. Kweli nawaambia, atamweka juu ya vitu vyake vyote.
45. Lakini, mtumwa yule akisema moyoni mwake, Bwana wangu anakawia kuja, akaanza kuwapiga wajoli wake, wanaume kwa wanawake, akila na kunywa na kulewa;