9. Wewe uuhubiriye Sayuni habari njema,Panda juu ya mlima mrefu;Wewe uuhubiriye Yerusalemu habari njema,Paza sauti kwa nguvu;Paza sauti yako, usiogope;Iambie miji ya Yuda, Tazameni, Mungu wenu.
10. Tazameni, Bwana Mungu atakuja kama shujaa,Na mkono wake ndio utakaomtawalia;Tazameni, thawabu yake i pamoja naye,Na ijara yake i mbele zake.
11. Atalilisha kundi lake kama mchungaji,Atawakusanya wana-kondoo mikononi mwake;Na kuwachukua kifuani mwake,Nao wanyonyeshao atawaongoza polepole.
12. Ni nani aliyeyapima maji kwa konzi ya mkono wake, na kuzikadiri mbingu kwa shubiri, na kuyashika mavumbi ya dunia katika pishi, na kuipima milima kwa uzani, na vilima kama kwa mizani?
13. Ni nani aliyemwongoza roho ya BWANA, na kumfundisha kwa kuwa mshauri wake?
14. Alifanya shauri na nani, ni nani aliyemwelimisha na kumfunza njia ya hukumu, na kumfunza maarifa, na kumwonyesha njia ya fahamu?
15. Tazama, mataifa ni kama tone la maji katika ndoo, huhesabiwa kuwa kama mavumbi membamba katika mizani; tazama, yeye huvinyanyua visiwa kama ni kitu kidogo sana.