10. Tazameni, Bwana Mungu atakuja kama shujaa,Na mkono wake ndio utakaomtawalia;Tazameni, thawabu yake i pamoja naye,Na ijara yake i mbele zake.
11. Atalilisha kundi lake kama mchungaji,Atawakusanya wana-kondoo mikononi mwake;Na kuwachukua kifuani mwake,Nao wanyonyeshao atawaongoza polepole.
12. Ni nani aliyeyapima maji kwa konzi ya mkono wake, na kuzikadiri mbingu kwa shubiri, na kuyashika mavumbi ya dunia katika pishi, na kuipima milima kwa uzani, na vilima kama kwa mizani?
13. Ni nani aliyemwongoza roho ya BWANA, na kumfundisha kwa kuwa mshauri wake?