Isa. 40:1-11 Swahili Union Version (SUV)

1. Watulizeni mioyo, watulizeni mioyo, watu wangu, asema Mungu wenu.

2. Semeni na moyo wa Yerusalemu, kauambieni kwa sauti kuu ya kwamba vita vyake vimekwisha, uovu wake umeachiliwa; kwa kuwa amepokea kwa mkono wa BWANA adhabu maradufu kwa dhambi zake zote.

3. Sikiliza, ni sauti ya mtu aliaye,Itengenezeni nyikani njia ya BWANA;Nyosheni jangwani njia kuu kwa Mungu wetu.

4. Kila bonde litainuliwa,Na kila mlima na kilima kitashushwa;Palipopotoka patakuwa pamenyoka,Na palipoparuza patasawazishwa;

5. Na utukufu wa BWANA utafunuliwa,Na wote wenye mwili watauona pamoja;Kwa kuwa kinywa cha BWANA kimenena haya.

6. Sikiliza, ni sauti ya mtu asemaye, Lia!Nikasema,Nilie nini? Wote wenye mwili ni majani,Na wema wake wote ni kama ua la kondeni;

7. Majani yakauka, ua lanyauka;Kwa sababu pumzi ya BWANA yapita juu yake.Yakini watu hawa ni majani.

8. Majani yakauka, ua lanyauka;Bali neno la Mungu wetu litasimama milele.

9. Wewe uuhubiriye Sayuni habari njema,Panda juu ya mlima mrefu;Wewe uuhubiriye Yerusalemu habari njema,Paza sauti kwa nguvu;Paza sauti yako, usiogope;Iambie miji ya Yuda, Tazameni, Mungu wenu.

10. Tazameni, Bwana Mungu atakuja kama shujaa,Na mkono wake ndio utakaomtawalia;Tazameni, thawabu yake i pamoja naye,Na ijara yake i mbele zake.

11. Atalilisha kundi lake kama mchungaji,Atawakusanya wana-kondoo mikononi mwake;Na kuwachukua kifuani mwake,Nao wanyonyeshao atawaongoza polepole.

Isa. 40